NDOA NI NINI?
Ndoa ni muungano kati ya mwanamke na mwanamume kuishi pamoja kama mume na mke muda wote wa maisha yao. (Sheria ya ndoa – mwaka 1971 kifungu cha 9).
i) Wanaooana wawe wamekubaliana pasipo kulazimishwa na mtu.
ii) Ndoa ni ya mwanamke na mwanamume.
iii) Ni ndoa ya kudumu maishani.
Mpango na utaratibu wa MUNGU kwa wanandoa umewekwa wazi katika kitabu cha Mwanzo.
“Bwana MUNGU akasema si vema mtu huyu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufafana naye”. Mwanzo 2:18.
Hapa tunaona kuna suala la mamlaka katika ndoa, kwamba mke ni msaidizi.
“Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja”. Mwanzo 2:24.
Hapa tunaona kusudi la MUNGU katika suala
 la kuachana na kuambatana. Wanandoa wanatakiwa kuachana na wazazi wao 
katika maeneo matatu.
i) Kimwili – wawe na makazi yao wenyewe
ii) Kihisia – wategemeane na kutiana moyo na kusaidiana
iii) Kiuchumi – wajitegemee kwa mahitaji yao ya kila siku.
TENDO LA NDOA
Ukizingatia kanuni za MUNGU kibiblia kuhusu tendo la ndoa kwa wanandoa;-
i) Ni tukio dogo lenye umuhimu mkubwa.
ii) Kusudi kubwa la tendo la ndoa ni uzazi.
iii) Ni kinga dhidi ya majaribu.
iv) Ni burudani/starehe.
v) Ni suala la kuwa na uvumilivvu na kujitoa.
NDOA -TAASISI TAKATIFU
Ndoa yenye furaha na kuheshimika ni ile 
ambayo kila mmoja anafahamu na kutimiza wajibu wake katika ndoa kwa 
mujibu wa nafasi yake. Na hii ndio sharti la msingi kutupelekea kwenye 
ndoa yenye mafanikio.
i) Kumheshimu mwenzi wako kutokana na hadhi aliyonayo kama MUNGU alivyoagiza.
ii) Heshima inasaidia kutuepusha na ubinafsi na kuongozwa na hisia.
iii) Heshima katika ndoa inachochea mapenzi.
NDOA NI KUTOA
1. Ndio sio mkataba wa kijamii bali agano
 la kiroho. Waefeso 5:31-33 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na 
mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. Siri
 hiyo ni kubwa, ila mimi nanena habari ya KRISTO  na Kanisa. Lakini kila
 mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe, wala mke asikose 
kumstahi mumewe.
Hapa tunajifunza
i) Ndoa ni fumbo la ajabu la kiroho linalowaunganisha watu wawili, mwanamume na mwanamke (mst.31)
ii) Ndoa ya kikristo inaliganishwa na uhusiano uliopo kati ya KRISTO na Kanisa (mst.32)
iii) Mpango wa MUNGU katika ndoa unahitaji upendo wa kujitoa sadaka kama KRISTO anavyofanya kwa Kanisa (mst.33)
2. Ndoa ya Kikristo ni kujitoa sio 
kupokea. Wafilipi 2:3-4 Msitende neno lolote kwa kushindana wala kwa 
majivuno, bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenzie kuwa bora 
kuliko nafsi yake mwenyewe. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, 
bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.
Hapa tunajifunza
i) Kutokuwa wabinafsi
ii) Unyenyekevu
iii) Roho ya kutoa na kujitoa.
Wewe mume/mke, mahusiano yako na mwenzi 
wako yakoje? Unampenda mwenzi wako kama KRISTO anavyolipenda Kanisa 
lake?  Kama wewe ni mmojawapo wa wasiofuata kielelezo cha KRISTO katika 
ndoa usijisikie vibaya kwani hakuna aliye mkamilifu. Hata hivyo wajibu 
huu haukwepeki kwani ni agizo la MUNGU na lazima kutii maagizo yake, 
kumpenda MUNGU kwa moyo waklo wote na kwa roho yako yote na kwa akili 
zako zote na kwa nguvu zako zote. Na kumpenda jirani yako kama nafsi 
yao. Marko 12:30-31. Hivyo, hii ni nafasi yako ya kumwonyesha mwenzi 
wako upendo ambao wa muda mrefu ameukosa, upendo ambao KRISTO ameuonyesa
 kwa kanisa lake.
Barikiwa sana.
Comments
Post a Comment